MTUHUMIWA wa kesi ya ugaidi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama
Chadema Wilfred Lwakatale amefutiwa mashtaka yanayomkabili na kukamatwa
tena,kisha akafungulia mashtaka upya.
Kufutwa kwa mashtaka ya Lwakatale inatokana na makosa yaliyofanywa na upande
wa serikali, na kumfanya DPP kufuta mashtaka hayo.
Baada ya kuwasilishwa kwa hati hiyo ya DPP, Hakimu Mchauru alikubaliana nayo
na kuwafutia mashtaka washtakiwa hao waliokuwa wanakabiliwa na kesi namba 37 ya
mwaka 2013, iliyokuwa na mashtaka manne.
Mashtaka hayo ni pamoja na kula njama ya kutenda kosa la kutaka
kumdhuru Dennis Msacky kwa sumu, kushiriki kupanga njama za utekaji nyara,
kushiriki katika mkutano wa kupanga kitendo cha ugaidi cha utekaji nyara na
kuhamasisha vitendo vya ugaidi.
Washtakiwa hao wa kesi ya ugaidi walisomewa mashtaka hayo na kurudishwa
lumande mpaka April 3 mwaka huu kesi hiyo itakapo somwa tena mahakamani
hapo,hata hivyo washtakiwa hao walinyimwa dhama na kutokuruhusiwa kusungumza
chochote kwakuwa Mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi za ugaidi.
No comments:
Post a Comment