Saturday, January 19, 2013

TAARIFA YA MAENDELEO YA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA KUSOMESHA VIIJANA WENYE UWEZO KIMASOMO SHULENI WANAOTOKA KATIKA FAMILIA ZISIZO NA UWEZO

Hapa mjumbe wa MDI Dr. Frank akitafakari jambo wakati wa mazungumzo na mlezi wa wanafunzi Magu Sekondari

Mlezi wa Vijana Magu Sekondari Mwalimu Biseco

Wajumbe wa MDI kutoka kulia, King sele na Dr. Frank H. Mganga wakimsikiliza kwa makini Mlezi wa vijana Magu Sekondari Mwalimu Biseco

Wajumbe wa Kamati ya MDI kutoka kushoto ni Dr. Frank H. Mganga na King sele Kulia





Mjumbe wa MDI King sele akifuatilia jambo katika document ambayo inaonesha wanafunzi mbalimbali katika shule ya Magu Sekondari

Wajumbe wa MDI wakiwa na Mlezi wa vijana Mwalimu Biseco



UTANGULIZI

Umoja wa Wanamagu ni umoja wa Hiari, usio wa Kiserikali, usio wa Kisiasa wala wa kutengeneza faida, wenye malengo ya jumla ya kuwaweka pamoja wananchi wote wa Wilaya ya Magu iliyoko Mkoa wa Mwanza Tanzania kwa dhumuni la Kuelemisha na Kuhamasisha wananchi kuendeleza Utamaduni na Tabia ya kufanya Kazi kwa ushirikikiano unaojenga uwezo wa kujitegemea na kuleta mabadiliko ya maisha bora kwa watu wote katika familia na jamii kwa ujumla ili kujenga Amani,Umoja, Haki, Udugu, Demokrasia, Elimu, Uchumi, Utawala Bora, na Mazingira Nadhifu katika Jamii.

WALENGWA
Walengwa wakubwa wa mpango huu ni wanafunzi watatu (3) wa sekondari za kawaida (O-level) wenye uwezo kimasomo darasani lakini wanaotoka katika familia zisizo na uwezo (Maskini)

UTEUZI WA WAJUMBE
Jumla ya wajumbe wawili (2) waliteuliwa kutafuta wanafunzi watatu (3) wa sekondari za kawaida (O-Level)wenye uhitaji wa kusomeshwa ambao wanatoka katika familia zisizo na uwezo lakini wenye uwezo shuleni ili wasomeshwe na wajumbe wa MDI. Wajumbe hao ni King Sele na Dr. Frank H. Mganga ambao walipewa muda mwezi mmoja (1) wa kutekeleza zoezi hilo.

UTEKELEZAJI
Wajumbe walianza kazi yao kwa kuzitembelea shule za sekondari za Magu Sekondari na Itumbili sekondari ambapo walibaini idadi ya wanafunzi sita (6) ambao walionekana kuwa na uhitaji kwa kukizi vigezo vilivyokuwa vimewekwa na wadau wa MDI. Kamati hii ilifika tena shule ya sekondari ya Magu tarehe 18/0/2013 nakukutana na wanafunzi hao, viongozi mbali mbali wakiwemo walimu wa shule hiyo na mlezi wa vijana katika shule hiyo.

HITIMISHO
Kama ilivyooneshwa hapo juu, soezi la upatikanaji wa wanafunzi hao linaendelea vizuri na wanafunzi wanatarajiwaa kuwa wamepatikana mpaka mwisho wa mwezi Januari 2013.


No comments:

Post a Comment