VIONGOZI mbalimbali wa kitaifa wameendelea kufika katika Hospitali ya Aga
Khan, Dar es Salaam ili kumjulia hali Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya
Jinai (DCI) Robert Manumba, ambaye amelazwa katika chumba cha Wagonjwa Mahututi
(ICU).
Mke wa Waziri Mkuu, Tunu Pinda, Ofisa Mwandamizi Mstaafu wa Jeshi la Polisi,
Jamal Rwambow ni miongoni mwa viongozi ambao walifika hospitalini hapo jana na
kupata fursa ya kumwona Manumba, wakati juzi Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib
Bilali naye alimtembelea.
Viongozi wengine ambao wamemtembelea Manumba ni pamoja na Rais Jakaya
Kikwete na mke wake, Mama Salma Kikwete.
Wengine ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi, Naibu wake
Pereira Silima, Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa, Mkuu waJeshi la
Polisi nchini, Said Mwema pamoja na maofisa wengine wa vyeo vya juu wa jeshi
hilo.
Taarifa iliyotolewa jana na uongozi wa Hospitali ya Aga Khan, imeeleza kuwa DCI Manumba bado anaendelea kutibiwa akiwa chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari na wauguzi.
Taarifa iliyotolewa jana na uongozi wa Hospitali ya Aga Khan, imeeleza kuwa DCI Manumba bado anaendelea kutibiwa akiwa chini ya uangalizi wa karibu wa madaktari na wauguzi.
“Uongozi wa Hospitali ya Aga Khan unapenda kuujulisha umma kwamba Mkurugenzi
wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini, (DCI) Robert Manumba bado yupo
hospitalini, ambapo anaendelea kupatiwa matibabu.
“Hali ya afya yake bado inahitaji uangalizi wa karibu wa madaktari na
wauguzi,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.
Mganga Mkuu wa hospitali hiyo, Dk Jaffer Dharsee alisema kwamba kesho
atazungumzia kwa kina kuhusu matatizo yanayomsumbua Manumba hasa baada ya
majibu ya vipimo alivyofanyiwa juzi na jana.
Dk Dharsee alithibitisha kubaini kuwa Manumba anasumbuliwa na malaria kali
baada ya kumfanyia uchunguzi, ambapo baada ya kupatiwa huduma ya matibabu ya
awali hali yake ilianza kutoa faraja. Ilielezwa kuwa kutokana na Manumba
kutojitambua imeshindikana kumsafirisha kwenda kutibiwa nje ya nchi ingawa
haikutajwa ni nchi gani ambayo angepelekwa kwa matibabu ya uhakika ili kunusuru
uhai wake.
No comments:
Post a Comment