KUNAMAVAZI mengi na ya kila aina yanayovaliwa na wanawake mbalimbali duniani
lakini vazi la hijabu ni vazi pekee lenye sifa ya kutunza mwili wa mwanamke.
Kumekuwa na kawaida ya watu wengi kuamini kuwa vazi la nikabu na
hijabu ni kwaajili ya waislamu,leo naomba niseme kwamba siyo lazima
anayevaaa nikabu na hijabu awe ni muumini wa kislamu.
Unatakiwa kuelewa kwamba kuvaa stara si kwa muislamu bali kila mwanamke
anatakiwa kuvaa nguo inayofunika maungo ya mwili wake ili kuweka mwili wake
katika mazingira mazuri.
Maria Sadock ni mmoja kati ya wanaweka wa Kiristo ambaye anavaa hijabu na
nikabu ili kufanya ngozi yake isipigwe na jua na kuifanya kuwa nyororo. Sadock
alisema kwa kipindi kirefu alikuwa akitafuta jinsi ya kufanya mwili wake kuwa
na rangi moja pamoja na ngozi nyororo.
“Nilikuwa nikiangaika na mwili wangu wakati mwingine nilikuwa nikishangaa
kuona rangi mbili nikadhani nina tatizo ila baadae nikagundua kuwa mwili
ukiuacha wazi sana jua linaunguza ngozi,”alisema Sadock.
Katika hali ya kawaida wanawake wengi wameshindwa kutunza mili yao na
kuiweka kwenye muonekano mmoja na kudhani kuwa kupaka kemikali kutaweza kufanya
ngozi zao kuwa nyororo.
![]() |
|
Mwonekano wa vazi la hijabu kwa mwanamke |
Nivyema kutafuta njia zilizo salama katika kutunza miili yenu kwani kupaka
vitu vyenye kemikali husababisha madhara makubwa katika ngozi na mara nyingine
uleta magonjwa ya kansa na magonjwa mengine ya ngozi.
Kuhifadhi mwili kwa nguo zenye stara pia humsaidia mwanamke aonekane mwenye
heshima kwani hajaacha maungo yake wazi.
Kuna njia nyingine nyingi kama kuvaa shuruali na soksi huku kwa juu ukiwa
umevaa shati lenye mikono mirefu pia husaidia kuweka mwili kuwa na rangi moja
kutokana na sehemu hizo kutokuwa wazi.

No comments:
Post a Comment