MKURUGENZI wa Ulinzi na Usalama wa Chadema atapandishwa kizimbani leo kwa
mara ya pili kwa ajili ya Hakimu kutoa uamuzi endapo atapata dhamana baada ya
juzi dhamana yake kufungwa kutokana na kwamba anakabiliwa na kesi ya ugaidi.
Akisoma hati ya mashtaka juzi mbele ya Hakimu Mkazi, Emillius Mchauru,
Wakili wa Serikali Mkuu, Puldens Rweyongeza Wakili wa serikali alidai kuwa
Lwakatale na mwenzake Ludovic Joseph , Desemba 28,2012 walishirikiana kupanga
njama za utekaji nyara dhidi ya Msacky kinyume na kifungu cha 21 cha sheria
inayopinga ugaidi.
Katika shtaka la tatu, washtakiwa hao wanadaiwa kufanya mkutano wa vitendo
vya kigaidi kinyume na kifungu cha 5 (a) cha sheria namba 21 inayopinga ugaidi
iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.
Aliendelea kudai kuwa siku hiyo ya tukio, washtakiwa hao walipanga na
kushiriki katika mkutano wa kupanga kitendo cha ugaidi cha utekaji nyara dhidi
ya Msacky.
Kwa mujibu wa shtaka la nne, Lwakatale anadaiwa kuhamasisha vitendo vya ugaidi.
Kwa mujibu wa shtaka la nne, Lwakatale anadaiwa kuhamasisha vitendo vya ugaidi.
Aliongeza kudai kuwa siku hiyo ya tukio, Lwakatale akiwa mwenye nyumba,
akijua , aliruhusu mkutano kati yake na Ludovick ufanyike katika nyumba yake
kwa lengo la kuhamasisha vitendo vya kigaidi dhidi ya Msacky. Baada ya
kumaliza kusoma mashtaka hayo, washtakiwa hawakuruhusiwa kujibu chochote kwa
sababu Mahakama ya Hakimu Mkazi haina uwezo wa kusikiliza kesi hiyo hadi
Mahakama Kuu na wakili wa Serikali alidai kuwa kesi hiyo haina dhamana.
Pia aliiomba mahakama kuruhusu mshtakiwa Ludovick kupelekwa polisi kuendelea
na shughuli za upelelezi.Lwakatale anatetewa na mawakili, Peter Kibatara,
Mabere Marando, Abdallah Safari, Nyaronyo Kichere na Tundu Lisu.
![]() |
Lwakatale mbele (kushoto) na Ludovic mwenye shati nyeusi
wakiwa chini ya ulinzi mkali wa Askari Polisi jana kisutu |
Wakili wa utetezi Kibatara aliiomba mahakama kutoa dhamana kwa mteja wao
kulingana na mazingira husika na kwamba izingatie kuwa dhamana ni haki ya
msingi ya washtakiwa. Kibatara alidai kuwa ugaidi siyo kosa dogo ni kitu
kikubwa iwapo chombo cha kisheria kinachukua haki ya mtu ya dhamana ni lazima
kuwepo na sababu zinazojitosheleza kuwa mtu huyu kweli ni hatari na mahakama
iridhie kweli ni hatari anyimwe dhamana.
![]() |
Wafuasi wa Chadema wakionyesha ishara ya vidole viwili katika
chumba cha Mahakama ya Hakimu mkazi kisutu jana jijini Dar es Salaam |
Wakili Lisu aliunga mkono hoja za wakili Kibatara. Kwa upande wa wakili
Abdallah Safari aliitaka mahakama ichukue kumbukumbu kuwa vitendo vya
kubambikia kesi watu vimekithiri katika nchi hii. Hakimu Mchauro atatoa uamuzi
juu ya hoja hizo Jumatano ya Machi 20 leo, mwaka huu kama washtakiwa hao watapata
dhamana ama la.
No comments:
Post a Comment