Monday, March 18, 2013

Lwakatale ashtakiwa kwa ugaidi,anyimwa dhamana

MKURUGENZI wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilfred Lwakatale amenyima dhama katika kesi yake ya Ugaidi ilisomwa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Katika kesi hiyo Lwakatale na mwenzake Ludovick Rwezahura Joseph wamefikishwa katika Mahakama wakikabiliwa na mashtaka manne likiwemo la kula njama ya kutenda kosa la jinai la kutoa sumu kwa nia ya kumdhulu Dennis Msacky.
Akisoma hati ya mashtaka leo mbele ya Hakimu Mkazi, Emillius Mchauru, Wakili wa Serikali Mkuu, Puldens Rweyongeza kuwa washtakiwa hao walifanya kosa la kula njama na kutenda makosa ya jinai kinyume na kifungu cha 384 cha sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho 2002.
Mshtakiwa wa pili katika kesi ya Lwakatale Ludovick Rwezahura Joseph aliyenyoosha vidole viwili
Rweyongeza alidai kuwa Desemba 28, mwaka jana katika eneo la King’ong’o Wilaya ya Kinondoni, washtakiwa hao kwa pamoja walikula njama kwa kutoa sumu kwa nia ya kumdhulu Dennis Msacky kinyume na kifungu cha 227 cha sheria ya kanuni ya adhabu. Wakili huyo wa serikali katika shtaka la pili alidai kuwa washtakiwa hao kwa pamoja walikula njama ya kufanya kosa la jinai kinyume na kifungu cha sheria cha 24 (2) cha sheria dhidi ya ugaidi sura ya 21 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

No comments:

Post a Comment