Monday, March 18, 2013

Msafara wa Rais Kikwete Dar waua askari

MSAFARA wa Rais Jakaya Kikwete ambaye yupo katika ziara yake ya kikazi jijini Dar es Salaam umedaiwa kusababisha kifo cha askari wa usalama barabarani Kopro Elikiza Nko aliyekuwa akiongoza magari eneo la barabara ya new Bagamoyo mkabala na ofisi za TBC na Barabara ya Shekilango.
Habari zimeeleza kuwa msafara huo ulikuwa na magari yasiypungua 40 ikiwa katika mwendo kasi jambo ambalo lilichangia kwa kiasi kikubwa kutokea kwa ajali hiyo.
Shuhuda mmoja aliyetupasha habari amesema askari huyo kabla ya msafara kuanza kupita alisimamisha magari yaliyokuwa upande mwingine na  baada ya magari hayo kusimama naye aliondoka eneo la barabara na kupisha msafara huo.
"Trafic huyo baada ya kuona muda unazidi kwenda na magari yanazidi kuongezeka alihisi labda msafara wa Rais umeshamalizika ila magari yanayoendelea kwenda ni yaliyounga kwenye msafara huo jambo ambalo ni kinyume na sheria"alisema shuhuda wa ajali hiyo"nakuongeza:
"Baada ya kuingilia kati na kuanza kuruhusu gari za upande mwingine ndipo ilipotokea gari ambayo ilikuwa kwa kasi sana na kusababisha ajali hiyo ambapo marehemu aliweza kufariki palepale.
Shuhuda huyo amesema kilichowashangaza wengi ni kuona kuwa gari za msafara wa rais zimesababisha kifo lakini hazikusimama ili kutoa msaada kwa askari huyo badala yake ziliendelea na ziara hiyo".
Wasamaria wema wakiufunika mwili wa askari aliyegongwa na gari kwenye msafara wa rais na kufariki hapohapo
 Akizungumza na waandshi wa habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni,Charles Kenyela alikiri kuwepo kwa taarifa hizo na kusema kwamba askari huyo aligongwa na gari ambalo haikuwa kwenye msafara huo. "Nikweli askari huyo amefariki katika ajali hiyo, lakini hakugongwa na gari iliyokuwa kwenye msafara bali ajali hiyo imesababishwa na gari aina Land Rova inayomilikiwa na Kanisa la Assemblies Of God (TAG) na tayari jeshi la polisi limeanza kumtafuta dereva wa gari hilo"alisema Kenyela.

No comments:

Post a Comment