![]() |
Mwenyekiti wa Chadema Taifa Freeman Mbowe akihutubia mkutano wa hadhara hivi karibuni |
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia
na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe amekanusha vikali kwamba tukio lililomkuta
Mwandishi wa habari Absalom Kibanda halikufanywa na chama chake bali watu
wasio na mapenzi mema na chama hicho wamelenga kukipaka matope.
Akizungumza wakati akiwahutubia
mamia ya watu kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Shycom
mkoani Shinyanga Mbowe amesema mpango wa uchochezi na utekaji aliofanyiwa
Kibanda usihusishwe na suala la mwanachama wake Alfred Lwakatare.
"Sisi hatunamuda wa kumteka
mtu, watu wanadai kuwa tumemteka Kibanda, ili iweje sasa, hatuna kikosi
chochote cha silaha, hawa ni baadhi ya watu wanaotaka kukipaka matope
chama,"alisema Mbowe.
Aidha Mbowe alierndelea kutoa hisia
zake kuwa hoja yao ya kutaka kufanya maandamano nchini nzima ili waziri wa
Elimu ajiuzulu ipo palepale na kwamba kwa sasa wapo katika maandalizi.
No comments:
Post a Comment