Monday, March 11, 2013

TAARIFA YA MAENDELEO YA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA KUSOMESHA VIIJANA WENYE UWEZO KIMASOMO SHULENI WANAOTOKA KATIKA FAMILIA ZISIZO NA UWEZO



UTANGULIZI


Umoja wa Wanamagu ni umoja wa Hiari, usio wa Kiserikali, usio wa Kisiasa wala wa kutengeneza faida, wenye malengo ya jumla ya kuwaweka pamoja wananchi wote wa Wilaya ya Magu iliyoko Mkoa wa Mwanza Tanzania kwa dhumuni la Kuelimisha na Kuhamasisha wananchi kuendeleza Utamaduni na Tabia ya kufanya Kazi kwa ushirikikiano unaojenga uwezo wa kujitegemea na kuleta mabadiliko ya maisha bora kwa watu wote katika familia na jamii kwa ujumla ili kujenga Amani,Umoja, Haki, Udugu, Demokrasia, Elimu, Uchumi, Utawala Bora, na Mazingira Nadhifu katika Jamii.
 
Wanafunzi wenye uhitaji wa kusomeshwa kutoka shule ya Sekondari Itumbili. Kutoka kushoto ni Anastazia Costantine, Samuel Wanga na Emanuel Wilson Maningu walipokutana na wanakamai wa MDI










Hapa wanakamati wetu wakiwa wamefika katoka shule ya Sekondari Itumbili na kukutana na Mwalimu Seif ambaye alikuwa anakaimu Madaraka ya Mwalimu Mkuu wa shule. Kushoto kabisa ni Dr Frank Mganga na Kulia kabisa ni King Sele



WALENGWA
Walengwa wakubwa wa mpango huu ni wanafunzi watatu (3) wa sekondari za kawaida (O-level) wenye uwezo kimasomo darasani lakini wanaotoka katika familia zisizo na uwezo (Maskini)

 
UTEUZI WA WAJUMBE
Jumla ya wajumbe wawili (2) waliteuliwa kutafuta wanafunzi watatu (3) wa sekondari za kawaida (O-Level)wenye uhitaji wa kusomeshwa ambao wanatoka katika familia zisizo na uwezo lakini wenye uwezo shuleni ili wasomeshwe na wajumbe wa MDI. Wajumbe hao ni King Sele na Dr. Frank H. Mganga.



Hapa ni wakati mazungumzo yakiendelea kati ya wanakati King Sele Kulia na Dr. Frank katikati na mwanafunzi Samueli Wanga



Wanakamai na mwanafunzi wakiendelea na mazungumzo zaidi

Dr Frank na King Sele wakichukua Taarifa za Mwanzafunzi Wanga




Mwanafunzi Anastazia Costantine

Mwanafunzi Emanuel Wilson Maningu


UTEKELEZAJI
Wajumbe walianza kazi yao kwa kuzitembelea shule za sekondari za Magu Sekondari na Itumbili sekondari ambapo walibaini idadi ya wanafunzi sita (6) ambao walionekana kuwa na uhitaji kwa kukizi vigezo vilivyokuwa vimewekwa na wadau wa MDI. Kamati hii ilifika tena shule ya sekondari ya Magu tarehe 18/01/2013 nakukutana na wanafunzi hao, viongozi mbali mbali wakiwemo walimu wa shule hiyo na mlezi wa vijana katika shule hiyo. Tarehe 18/02/2013 kamati ilifika shule ya Sekondari Itumbili na kukutana na wanafunzi wenye uhitaji.

Mwanakamati King Sele


Mwanakamati Dr Frank H Mganga


King Sele


Dr. Frank H Mganga

Mwanafunzi Samwel Wanga


Mwanafunzi Samuel Wanga


Dr Frank Mganga




Dr Frank akiwa na Kaimu Mkuu wa shule ya Sekondary Itumbili

Wanakamati waliteta jambo na Kaimu Mkuu wa Shule ya Itumbili




HITIMISHO
Kama ilivyooneshwa hapo juu, zoezi la upatikanaji wa wanafunzi hao linaendelea vizuri na wanafunzi wanatarajiwaa kuwa wamepatikana mpaka mwisho wa mwezi Machi.

 

 










No comments:

Post a Comment