Monday, May 13, 2013

Mo Ibrahim Foundation MSc Scholarship in Governance and State-building in UK, 2013

Mo Ibrahim Foundation is funding one MSc Scholarship in Governance and State-building to start in September 2013 at University of Birmingham, UK. Student must have a first class honors or equivalent degree. English proficiency is required. African nationals are eligible for this scholarship. Preference is given to nationals of sub-Saharan African countries. Applicants have an opportunity of a six-month internship at IDD and six months with the Mo Ibrahim Foundation in London with a full scholarship.

Study Subject(s):
The scholarship is provided to study MSc in governance and state-building at University of Birmingham in UK.

Course Level:
This scholarship is for pursuing Master’s-MSc degree level at University of Birmingham.

Scholarship Provider: Mo Ibrahim Foundation

Scholarship can be taken at: UK
Eligibility:
 -The entry requirements consist of: -1st class Honors degree or equivalent from an approved university. Adequate capacity in written and spoken English.
-For those whose first language is not English, evidence of this capacity is required.
-Applicants should reach at least level 6.5 in the IELTS or 580 /93 for TOEFL. Please check the University website for more information on English language requirements.
-Experience in economics and statistics, demonstrated through a good mark received for at least one course at undergraduate level.
-Applicants must be African nationals domiciled (or permanent residents) in an African country.
-Preference will be given to scholarship candidates living in Sub-Saharan Africa.
Scholarship Open for Students of Following Countries:
 Nationals of Africa (Algeria, Angola, Benin, Botswana, Burkina Faso, Burundi, Cameroon, Cape Verde, Central African Republic, Chad, Comoros, Congo-Brazzaville, Congo-Kinshasa, Cote d’Ivoire, Djibouti, Egypt, Equatorial Guinea, Eritrea, Ethiopia, Gabon, Gambia, Ghana, Guinea, Guinea Bissau, Kenya, Lesotho, Liberia, Libya, Madagascar, Malawi, Mali, Mauritania, Mauritius, Morocco, Mozambique, Namibia, Niger, Nigeria, Rwanda, Senegal, Seychelles, Sierra Leone, Somalia, South Africa, South Sudan, Sudan, Swaziland, São Tomé and Príncipe, Tanzania, Togo, Tunisia, Uganda, Western Sahara, Zambia, Zimbabwe) can apply for this Master’s scholarship.

Scholarship Description:
The International Development Department is pleased to announce an exciting opportunity to undertake the MSc in Governance and State-building, followed by a six-month internship at IDD and six months with the Mo Ibrahim Foundation in London with a full scholarship. Applicants must have the equivalent of a first class UK bachelors degree and be African nationals domiciled (or permanent residents) in an African country. Preference will be given to scholarship candidates living in Sub-Saharan Africa. The Governance and State building programme is one of the specialized streams within international development, and takes an interdisciplinary standpoint, combining the theoretical rigor of political economy and the practical experience of development. The good governance agenda occurs now increasingly alongside debate on state-building, which encompasses issues such as accountability and transparency, corruption, conflict, political settlement, human rights, participation, access to justice and democratization. Governance and state-building are of particular interest to governments, non-governmental organizations and development agencies, as well as to a growing and vibrant academic community.

Number of award(s):
 Mo Ibrahim Foundation is providing one scholarship for our MSc in Governance and State building, to start in September 2013.

Duration of award(s):
The scholarship will be for a two-year programme, with the successful candidate undertaking the full MSc programme and then six months within the Foundation as an intern, based in London.

What does it cover? 
The scholarship includes:
1.Full tuition fee
2.Air fare to and from the United Kingdom and visa
3.Monthly stipend of £920 for 18 months
4.Arrival allowance of £920 The remaining six months for the internship will be funded directly to the successful candidate by the Mo Ibrahim Foundation.

Selection Criteria: Not Known
Notification: Not Known


How to Apply:
Applications must be received through the University online application system by the 31st May 2013. In addition to the usual documents to be submitted, applicants should also upload a 500 word statement and CV. This statement should set out why the applicant is the best candidate for the scholarship. Applicants must then send an email to Mrs Debra Beard (d.l.beard-at-bham.ac.uk) informing her of their wish to be considered for the Mo Ibrahim Scholarship and their ID number. Please include ‘Mo Ibrahim Scholarship’ in the subject line of the email.
Scholarship Application Deadline: The deadline for applications is 31st May 2013.

MALECELEA ATAHADHARISHA KUHUSU VURUGU ZINAZOENDELEA NCHINI


Waziri Mkuu Mstaafu John Malecela akifafanua jambo

Wakati Waziri Mkuu Mstaafu, John Malecela ameonya Watanzania kuhusu mpasuko wa kidini akibainisha kuwa utaigawa nchi vipande vipande, Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi ametoa wito maalumu akiwataka waumini wa dini tofauti kuvumiliana.

Malecela na Mwinyi walitoa kauli hizo mjini Dodoma na Kibaha, Pwani jana kwa nyakati tofauti, wote wakiwa na nia ya kusisitiza ulinzi wa amani ya nchi inayoanza kutetereka.
Kauli ya Malecela

Malecela alisema kwa namna ilivyo sasa, Tanzania imekuwa ni tofauti na ile aliyoanza kuiona yeye katika kipindi cha uhuru kwenye miaka ya 1960 wakati huo nchi ikiwa moja na watu wake wakiwa ni wamoja.

“Msipokuwa makini na amani yenu, nchi hii mtaigawa vipande vipande na kamwe amani ya kweli haiwezi kupatikana kwa mambo ya kusingiziana, badala yake tusaidiane sisi kwa sisi, na sisi na viongozi,” alisema.

Onyo la Malecela limekuja kutokana na mfululizo wa matukio ya uvunjifu wa amani na mpasuko wa kidini unaoanza kujitokeza nchini.

Malecela alieleza wasiwasi wake juu ya tofauti za kidini katika ibada maalumu ya kuombea amani iliyofanyika katika Kanisa Anglikana Chiwondo lililoko kijiji cha Hombolo katika Manispaa ya Dodoma.

Anafuata nyayo za viongozi wa kitaifa walioonya masuala ya udini kama Rais Jakaya Kikwete, Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein, Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Marais wastaafu, Mwinyi na Benjamin Mkapa pamoja na mawaziri wakuu wa zamani, Edward Lowassa na Frederick Sumaye.

Alisema waliovamia na kupiga bomu kanisani Arusha ambapo Balozi wa Vatican nchini, Francisco Montecillo Padilla alinusurika kuuawa, si wajinga na wanaweza kufanya mambo kama hayo eneo lolote nchini.

 “Kujenga nchi ni kazi ngumu sana lakini kuibomoa ni kitendo cha muda mfupi ambacho kinaweza kufanyika kwa kutumia sekunde chache ni lazima kuisaidia serikali katika kuitafuta amani,” aliongeza Malecela.

  Malecela ameonya baadhi ya watu kutochukua sheria mikononi kuhusu yale yanayowapata na badala yake waiachie Serikali yao kufanya uamuzi wa nini kifanyike ili amani ibaki.

Nasaha za Mwinyi

Kwa upande wake Rais Mstaafu Mwinyi alisisitiza amani idumishwe na kuwataka Waislamu na Wakristo kupendana na kuvumiliana ili jamii iweze kuishi bila hofu.

“Haiwezekani dini moja kuitaka dini nyingine isiwepo,” alisisitiza Mwinyi. Mwinyi alitoa msisitizo huo jana mjini Kibaha wakati akitoa mawaidha yaliyolenga kusisitiza amani nchini kufuatia matukio kadhaa yaliyoripotiwa kutokea  nchini na kudaiwa yanahusiana na masuala ya kidini.

Alisema si ajabu kukuta hata sasa baadhi ya watu wameingiwa na hofu na waumini wakisikia kitu hata kama ni paka wanakimbia na kuacha mahubiri.

 “Hakuna sababu ya kutufikisha hapo jamani, mbona dini hazijaanza leo? Tangu enzi watu wanaabudu kila mtu kwa imani yake, watu wanaoana, wanakula pamoja, wapo ofisi moja, magari wanapanda pamoja sasa iweje hii itokee leo hii?” alihoji Mwinyi.

MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU AKATISHA UHAI WAKE

Mwanfunzi wa Chuo Kikuu aliyejinyonga Yobe Magongoninga Mfune (23)
MWANAFUNZI wa Chuo Kikuu cha Bunda kilichopo mijini Lilongwe nchini Malawi, amejinyongwa kwa kutumia mkanda wa begi lake la kusafiria. Mwanfunzi huyo aliyetambulika kwa jina la Yobe Magongoninga Mfune (23) alikatisha maisha yake huku sababu za kifo cha kikiwa siri kati yake na Mungu wake.

Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Malawi Rhoda Manjolo alisema kwamba, Mfune alikuwa mwanafunzi wa shahada ya kwanza katika fani ya utawala wa mazingira na maliasiri.
Manjolo alisema, marehemu alikutwa amejinyonga katika chumba chake kwenye hosteli za chuo hicho. Hata hivyo Polisi walisema kwamba, marehemu alikuwa na mahusiano na mwanamke mmoja aliyewahi kufanyakazi katika chuo hicho kwa siku za nyuma.

Msemaji wa Polisi nchini Malawi aliongeza kwamba, marehemiu alikuwa akiishi na rafiki yake katika chumba hicho ambaye aliondoka tangu may 6 mwaka huu na aliporudi akakuta mlango umefungwa kwa ndani ndipo alipoamuwa kutoa taarifa kwa uongozi wa chuo ambao waliamuwa kuvunja mlango huo kuingia ndani.

Alisema kwamba baada ya mlango huo kufunguliwa hawakuona mtu lakini walipofungua kabati la nguo wakakutana na mwili wa marehemu ukiwa unaning'ining'ia. "Uchunguzi wa madaktari unasema kwamba kifo cha mwanafunzi huyo kilitokana na msongo wa mawazo"alisema Manjolo.

Hata hiyo marafiki wa karibu wa mwanafunzi huyo walisema kwamba, siku chache kabla ya marehemu kufariki dunia aliwahi kuandika katika ukurasa wake wa Face Book kwamba "nitaweka historia nyingine mpya ambayo sijawai kuiweka tangu nilipozaliwa, na kumbukukumbu yake haitakaa ikafutika tena,na baada ya hapo sitajali wala kuwa na mahusiano na mambo yote ya hapa duniani, bali itakuwa juu yangu na Mungu wangu"ilisema sehemu ya status za marehemu.

TANZANIA YAHOFIA KUWA NA WAKATI MUGUMU KIMATAIFA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiriakiano wa Kimataifa Bernard Membe akifafanua jambo

TANZANIA iko hatarini kuingia katika mgogoro mkubwa wakidiplomasia dhidi ya nchi za Falme za Kiarabu (UAE) na Saudi Arabia kutokana na tuhuma za kigaidi zinazo wakabili raia wa nchi hizo.


Taarifa zilizonaswa na MDI Blog kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya nchini na Ushirikiano wa Kimataifa zinaeleza kwamba nchini hizo zimeanza kuihoji serikali uhalali wa kuwashirikilia raia wake.


Hatua ya kukamatwa kwa raia wa nchi hizo kwa tuhuma za ugaidi uliofanyika jijini Arusha katika Kanisa Katoliki Parokia ya Olasiti nje kidogo ya Jiji hilo ulioua watu watatu na kusababisha watu zaidi ya 62 kujeruhiwa viabaya ni ishara mbaya kwa mahusiano ya kidiplomasia.


"Serikali imepokea taarifa kutoka nchi hizo ikihoji uhalli wa raia wake kukamatwa kwa tuhuma za ugaini, hatua hii inaweza kuwa mbaya zaidi endapo itabainika kwamba watuhumiwa hao si magaidi, kwani masuala ya diplomasia baina ya Tanzania na nchi hizo inaweza kuwa mbaya zaidi, tena ukizingatia kwamba serikali inapata misaada mingi kutoka nchi hizo,kutokana na mahusiano mazuri baina yetu na wao"kilisema chanzo hicho.


Taarifa hizo pia zilidhibishwa na Waziri Bernard Membe wakati akizungumza na gazeti moja la kila siku nchini Tanzania ambaye leo anakwenda jijini Arusha kufuatilia suala hilo na hasa kwa kukamatwa raia wa kigeni wakihusishwa na tukio hilo, wakiwa ni miongoni mwa watu 12 wanaoshikiliwa na polisi wakituhumiwa kuhusika na shambulio hilo lililoua watu watatu na wengine zaidi ya 60 kujeruhiwa.


“Ninakwenda Arusha leo ili kufahamu undani wa suala hili. Baada ya kwenda ndiyo nitakuwa katika nafasi ya kuongelea mambo haya,” alisema Membe wakati alipoulizwa jana kuhusu malalamiko ya nchi za Saudi Arabia na Falme za Kiarabu (UAE) kuhusu kukamatwa kwa raia wao. Watu wanaoshikiliwa na polisi kwa tuhuma hizi ni pamoja nja Victor Ambrose Calist (20), Mwendasha Bodaboda na mkazi wa Kwa Mrombo, Jeseph Yusuph Lomayani (18) mwendesha Bodaboda, Mkazi wa Kwa Mrombo jijini  Arusha.


Wegine ni George Batholomeo Silayo (23), mfanyabiashara na mkazi wa Olasiti, Arusha, Mohamed Sulemani Said (38) mkazi wa Ilala, Dar es Salaam na Jassini Mbaraka (29) mkazi wa Arusha. Wale wanaotuhumiwa kutoka nje ya Tanzania ni pamoja na raia wa Falme za Kiarabu (UAE), Said Abdalla Said (28), Abdulaziz Mubarak (30) na Said Mohsen wakati Jassini Mbaraka (29) anatokea Saudi Arabia.


Tuesday, April 30, 2013

TAARIFA YA MKUTANO WA MAGU DEVELOPMENT INITIATIVE (MDI) ULIOKETI TAREHE 20 APRILI, 2013 MERRYLAND MWENGE DAR ES SALAAM

AGENDA

1.UTAMBULISHO WA WANACHAMA WALIOHUDHURIA;
2.KUHUSU KUSAJILI UMOJA WANAMAGU;
3.MAREKEBISHO YA KATIBA KABLA YA KUSAJILI;
4.MENGINEYO;

Mwenyekiti alifungua kikao cha MDI mnamo saa kumi na moja na nusu baada ya sala ambayo iliongozwa na mjumbe mmoja.

UTAMBULISHO WA WANACHAMA WALIOHUDHURIA
Wanachama walijitambulisha kwa majina na mahali wanapoishi pamoja na chimbuko lao katika Wilaya ya Magu, walifanya hivi mmoja baada ya mwingine mpaka idadi yao ilipokamilika, yaani wanachama 26 ambao ndio kimsingi walihudhuria kikao. Pia Mwenyekiti alitoa taarifa kuwa kikao hicho kilikuwa na dhumuni kuu moja la kupata majina ya wanachama na saini zao kwa ajili ya kukamilisha usajili wa umoja wa Wanamagu.


KUHUSU KUSJILI UMOJA WA WANAMAGU
Mwenyekiti alianza kwa kutoa historia fupi ya Magu Development Initiative, kuwa ilianzishwa mwaka 2009 na malengo yake ya msingi ni kuwaweka pamoja wanamagu waishio Dar es Salaam na Wanamagu wote waliotawanyika kokote duniani ili kushiriki katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na hatimaye kuleta maendeleo katika wilaya ya Magu.
Kutokea mwaka 2009 Umoja wa wanamagu haukuwahi kusajiliwa mpaka sasa ambapo kumekuwa na umuhimu mkubwa wa kuusajili ili kufanya kazi zake kisheria na kwa kuzingatia taratibu za nchi ya Tanzania kama sheria ya mashirika yasiyo ya kiserikali yaani NGOs ACT No. 24 of 2002 inavyoelekeza.

MAREKEBISHO YAKATIBA KABLA YA KUSAJILI
Wajumbe walikubaliana kupitia Katiba ya Umoja kifungu kwa kifungu na kuipiisha baada ya marekebisho machache kama ifuatavyo;

Kiingilio na Michango kwa Mwezi
Kila mwanachama atatakiwa kulipa Tshs. 50,000 kama kiingilio. Kila mwanachama atatakiwa kutoa sh 7,000 kwa kila mwezi; Tshs. 5,000 kwa ajili ya kuimalisha umoja na Tshs. 2,000 kwa ajili ya shughuli za kijamii. Pia mwanachama atapoteza haki ya uanachama pale tu atakaposhindwa kulipa ada ya mwezi kwa miezi mitatu mfululizo au kukosa kuhudhuria vikao vitatu mfulurizo.


Nembo
Wanachama walikubaliana kuendelea na nembo iliyopo kuwa inatosha. Pia kutakuwa na mhuri ambao utakuwa na alama ya nembo ya MDI 


Utambulisho wa Jumuiya
Wanachama walikubaliana kuwa makao makuu ya jumuia yatakuwa Mwenge Dar es salaam, na ofisi nyingi zitafunguliwa katika mikoa yote ya Tanzania. Pia kulikuwa na makubaliano ya kugawa jiji la Dar es salaam katika kanda mbalimbali kwa ajili ya kuwezesha wanachama kukutana kwa urahishi zaidi.

MAENGINEYO
1.       MSIBA
Kikao kilikubaliana kwamba mwanachama hai atapatiwa Tsh 200,000 kama atapatwa na msiba wa kufiwa na watu wafuatao;Baba , Mama, Mke au Mtoto.

2.       MATIBABU
Mwanachama atakayeugua na kuhitaji msaada wa kifedha kamati itampatia Tsh 100,000 kama mchango wa matibabu
Ajenda zingine zilihifadhiwa mpaka pale jumuia itaimalika nazo ni; ndoa, kukopeshana, kadi ya uanachama, uongozi wa kikanda

HITIMISHO
Baada ya kukubaliana kuyapitisha yaliyotajwa hapo juu, wajumbe walikubaliana kwa kauli moja kuwa, waiachie Kamati ya usajili ifanye kazi yake na itakuwa ikitoa taarifa kwa uongozi wa MDI mpaka usajili utakapokamilika.
Kikao kilifungwa kwa sala iliyoongozwa pia na mjumbe mmoja na Mwenyekiti alitoa kauli ya kufunga kikao kwa kusema kuwa, Mkutano mwingine utapangwa baada ya usajili kukamilika.

“Pamoja Tunajenga Magu yenye Maendeleo Endelevu”


Wednesday, April 17, 2013

Polisi Mwanza yawashikilia raia wawili wa Burundi

Mwanza.

Kutokana na kuenea kwa Dola Bandia za kimarekani katika maeneo mbalimbali nchini, Polisi MKoani Mwanza inawashilikilia raia wawili wa Burundi kwa tuhuma za kumiliki noti bandia za marekani 1100 zenye thamani ya pesa za kitanzania shilingi Milioni moja laki saba na themanini na mbili elfu.
Kukamatwa kwa raia hao wa Burundi kunafuatia polisi kupata taarifa kutoka kwa raia wema kuwa kuna watu wanamashaka nao.

Kamanda Mangu
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Kamishna Msaidizi Mwandamizi Ernest Mangu alisema raia hao wa Burundi walikamatwa maeneo ya uwanja wa ndege wakiwa kwenye gari lenye namba za usajili T 684 ACR.
Kuhusu gari hilo kumilikiwa na kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, Kamanda Mangu, taarifa hizo wanazifanyia kazi, japo kuwa uhalifu hauna chama
Kamanda Mangu alitoa hadhari kwa wafanyabiashara mkoani Mwanza kutokana na dola bandia za marekani kuzagaa
Polisi inawatafuta watu wengine wakihusishwa kushirikiana na raia hao wa Burundi kutekeleza uhalifu.