Monday, March 18, 2013

Lwakatale atinga Kortini,asomewa mashitaka manne

HATIMAYE Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema,) Wilfred Lwakatale amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam na kusomewa mashtaka manne.
Kada huyo wa Chadema  anashitakiwa kwa kosa la  ya kula njama ya kumteka na kumdhuru Denis Msacky na amenyimwa dhama katika kesi yake ya Ugaidi ilisomwa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Katika kesi hiyo Lwakatale na mwenzake Ludovick Rwezahura Joseph wamefikishwa katika Mahakama wakikabiliwa na mashtaka manne likiwemo la kula njama ya kutenda kosa la jinai la kutoa sumu kwa nia ya kumdhulu Dennis Msacky.
Akisoma hati ya mashtaka leo mbele ya Hakimu Mkazi, Emillius Mchauru, Wakili wa Serikali Mkuu, Puldens Rweyongeza kuwa washtakiwa hao walifanya kosa la kula njama na kutenda makosa ya jinai kinyume na kifungu cha 384 cha sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho 2002.
Rweyongeza alidai kuwa Desemba 28, mwaka jana katika eneo la King’ong’o Wilaya ya Kinondoni, washtakiwa hao kwa pamoja walikula njama kwa kutoa sumu kwa nia ya kumdhulu Dennis Msacky kinyume na kifungu cha 227 cha sheria ya kanuni ya adhabu.
Wakili huyo wa serikali katika shtaka la pili alidai kuwa washtakiwa hao kwa pamoja walikula njama ya kufanya kosa la jinai kinyume na kifungu cha sheria cha 24 (2) cha sheria dhidi ya ugaidi sura ya 21 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.
Alidai kuwa washtakiwa hao, Desemba 28,2012 walishirikiana kupanga njama za utekaji nyara dhidi ya Msacky kinyume na kifungu cha 21 cha sheria inayopinga ugaidi.
Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema Wilfred Lwakatale akiwasalimia wafuasi wa chama hicho kwa ishara ya vidole viwili baada ya kuwasili katika chumba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Katika shtaka la tatu, washtakiwa hao wanadaiwa kufanya mkutano wa vitendo vya kigaidi kinyume na kifungu cha 5 (a) cha sheria namba 21 inayopinga ugaidi iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.
Aliendelea kudai kuwa siku hiyo ya tukio, washtakiwa hao walipanga na kushiriki katika mkutano wa kupanga kitendo cha ugaidi cha utekaji nyara dhidi ya Msacky. Kwa mujibu wa shtaka la nne, Lwakatale anadaiwa kuhamasisha vitendo vya ugaidi.

No comments:

Post a Comment