Aliyekuwa Ofisa Elimu
(Taaluma) Wilayani Magu Mkoani Mwanza Ndugu Kamili Paul Dusu amefariki dunia.
Habari kuroka Wilayani Magu zinasema, Ofisa Elimu huyo kabla ya kukutwa na umauti, alikuwa
kwenye kikao cha Kamati ya Elimu, Afya na Maji kilichokuwa kinafanyika Mjini
Magu.
Kifo hicho
kimethibitishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya ya Magu, Bi Naomi Nnko na
kusema kuwa, awali Ofisa Elimu Dusu alipokuwa kwenye kikao hicho alianguka
ghafla, hali iliyomsababishia kufikwa na umauti baadaye.
Alisema kuwa baada ya
kuanguka ukumbini, alipelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Magu, lakini hali
yake ilikuwa mbaya zaidi na kukimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando
Jijini Mwanza ambako alipoteza maisha jana (18/01/2013) alfajiri.
Aidha, alisema kuwa,
Ofisa Elimu huyo alikuwa akisumbuliwa na presha iliyokuwa inapanda na kushuka
mara kwa mara.
Safu ya uongozi wa
MDI, kwa niaba ya Wanamagu wote inawapa pole wale wote walioguswa na msiba huu
popote pale walipo.
Bwana katoa na Bwana
katwaa, jina lake lihimidiwe.
AMEN
No comments:
Post a Comment