AGENDA
1.UTAMBULISHO WA WANACHAMA WALIOHUDHURIA;
2.KUHUSU KUSAJILI UMOJA WANAMAGU;
3.MAREKEBISHO YA KATIBA KABLA YA KUSAJILI;
4.MENGINEYO;
Mwenyekiti alifungua kikao cha MDI mnamo saa kumi na moja
na nusu baada ya sala ambayo iliongozwa na mjumbe mmoja.
UTAMBULISHO WA
WANACHAMA WALIOHUDHURIA
Wanachama walijitambulisha kwa majina na mahali wanapoishi
pamoja na chimbuko lao katika Wilaya ya Magu, walifanya hivi mmoja baada ya
mwingine mpaka idadi yao ilipokamilika, yaani wanachama 26 ambao ndio kimsingi
walihudhuria kikao. Pia Mwenyekiti alitoa taarifa kuwa kikao hicho kilikuwa na
dhumuni kuu moja la kupata majina ya wanachama na saini zao kwa ajili ya
kukamilisha usajili wa umoja wa Wanamagu.
KUHUSU KUSJILI UMOJA
WA WANAMAGU
Mwenyekiti alianza kwa kutoa historia fupi ya Magu
Development Initiative, kuwa ilianzishwa mwaka 2009 na malengo yake ya msingi
ni kuwaweka pamoja wanamagu waishio Dar es Salaam na Wanamagu wote
waliotawanyika kokote duniani ili kushiriki katika shughuli mbalimbali za
kiuchumi na hatimaye kuleta maendeleo katika wilaya ya Magu.
Kutokea mwaka 2009 Umoja wa wanamagu haukuwahi kusajiliwa
mpaka sasa ambapo kumekuwa na umuhimu mkubwa wa kuusajili ili kufanya kazi zake
kisheria na kwa kuzingatia taratibu za nchi ya Tanzania kama sheria ya
mashirika yasiyo ya kiserikali yaani NGOs ACT No. 24 of 2002 inavyoelekeza.
MAREKEBISHO YAKATIBA
KABLA YA KUSAJILI
Wajumbe walikubaliana kupitia Katiba ya Umoja kifungu kwa
kifungu na kuipiisha baada ya marekebisho machache kama ifuatavyo;
Kiingilio na Michango
kwa Mwezi
Kila mwanachama atatakiwa kulipa Tshs. 50,000 kama kiingilio. Kila
mwanachama atatakiwa kutoa sh 7,000 kwa kila mwezi; Tshs. 5,000 kwa ajili ya
kuimalisha umoja na Tshs. 2,000 kwa ajili ya shughuli za kijamii. Pia mwanachama
atapoteza haki ya uanachama pale tu atakaposhindwa kulipa ada ya mwezi kwa miezi mitatu mfululizo au
kukosa kuhudhuria vikao vitatu mfulurizo.
Nembo
Wanachama walikubaliana kuendelea na nembo iliyopo kuwa
inatosha. Pia kutakuwa na mhuri ambao utakuwa na alama ya nembo ya MDI
Utambulisho wa Jumuiya
Wanachama walikubaliana kuwa makao makuu ya jumuia yatakuwa
Mwenge Dar es salaam, na ofisi nyingi zitafunguliwa katika mikoa yote ya
Tanzania. Pia kulikuwa na makubaliano ya kugawa jiji la Dar es salaam katika
kanda mbalimbali kwa ajili ya kuwezesha wanachama kukutana kwa urahishi zaidi.
MAENGINEYO
1. MSIBA
Kikao kilikubaliana kwamba mwanachama hai atapatiwa Tsh
200,000 kama atapatwa na msiba wa kufiwa na watu wafuatao;Baba , Mama, Mke au
Mtoto.
2. MATIBABU
Mwanachama atakayeugua na kuhitaji msaada wa kifedha kamati
itampatia Tsh 100,000 kama mchango wa matibabu
Ajenda zingine zilihifadhiwa mpaka pale jumuia itaimalika
nazo ni; ndoa, kukopeshana, kadi ya uanachama,
uongozi wa kikanda
HITIMISHO
Baada ya kukubaliana kuyapitisha yaliyotajwa hapo juu,
wajumbe walikubaliana kwa kauli moja kuwa, waiachie Kamati ya usajili ifanye
kazi yake na itakuwa ikitoa taarifa kwa uongozi wa MDI mpaka usajili
utakapokamilika.
Kikao kilifungwa kwa sala iliyoongozwa pia na mjumbe mmoja
na Mwenyekiti alitoa kauli ya kufunga kikao kwa kusema kuwa, Mkutano mwingine
utapangwa baada ya usajili kukamilika.
“Pamoja Tunajenga
Magu yenye Maendeleo Endelevu”