Saturday, January 19, 2013

VIONGOZI WA KIJIJI WASHIKILIWA KWA WIZI WA MAHINDI YA MSAADA



Mwenyekiti wa kijiji cha Mwibiti kata ya Ikoma Mkoani Tabora anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuiba Mahindi ya msaada yaliyotolewa na serikali kwa wananchi wa kijiji hicho. Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Suleimani Kumchaya ameeleza hayo alipokutana na waandishi wa Habari Mkoani humo.

Amesema kuwa tuhuma hiyo ya wizi wa mahindi, imetokea muda mfupi baada ya serikali kufikisha mahindi kiasi cha Tani 17 wilayani humo kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wanaokabiriwa na njaa. Amewataja viongozi wanaoshiikiliwa kwa tuhuma hizo za mahindi ya msaada kuwa ni Mwenyekiti wa Kijiji Hassan Ndimasalo, Katibu Mtendaji Mathew Masiyu, Suleimani Nassib, Joahari Nassor, Johari Hamis, na John Mhozya ambaye anaendelea kutafutwa.

Na Mdau wa MDI akiwa Tabora

No comments:

Post a Comment