Taarifa ya Helen Kijo-Bisimba- Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) Kuhusu Vurugu za Waislam na Wakristu Mkoani Geita
Tumepokea taarifa za masikitiko kuhusu vurugu zilizotokea huko Buselele
Chato kuhusu uchinjaji wa nyama unaobishaniwa na Waislam na
Wakristo.
Chanzo cha Habari hizi kimetueleza kuwa baada ya mivutano
kuhusu uchinjaji wa nyama .Baaadhi ya Wakristo waliamua kuanzisha bucha zao ili wachinje na kununua hapo ili wasishiriki kula nyama zilizochinjwa
kama sehemu ya ibada ya Kiislamu kwa vile uchinjaji kwa Waislam ni
ibada.
Baada ya kufungua Bucha hiyo leo asubuhi taarifa inasema watu
wanaosadikiwa kuwa waislam walifika kutaka kuifunga hiyo Bucha na
baadaye Polisi nao walifika na walitaka wamchukue mwenye bucha.
Suala hili likazua tafrani na pakatokea mapigano kati ya pande mbili
yaani waislam na wakristo na kuna watu wameumizwa.Taarifa imezidi
kueleza kuwa pia mali za aliyehamasisha
ufungwaji wa bucha nazo zimeharibiwa.
Baada ya kupokea taarifa hii
tumewatuma waangalizi wetu wa haki za binadamu kwenda kutuletea kwa kina
hali halisi kama watakavyoweza.Tunahabari kuwa kikosi cha kuzuia fujo
kilifika na kutuliza hizo vurugu.Jambo tunaloliona kwa haraka ni kuwa
kunaelekea kukosekana kwa uongozi wa kuyatazama masuala kama haya na
kuyawekea msimamo na maelekezo kabla vurugu kama hizi kutokea.
Pili
tunaona kuwa hali ya kukosa stahamala za kidini inajengeka nchini jambo
ambalo ni hatari sana kwa usalama na amani hapa nchini.
Wakati tunasubiri
taarifa zaidi tunapenda kutoa angalizo kwa viongozi wetu maana
tumesikia mkuu wa wilaya tayari ameshafika katika eneo la tukio,Masuala
kama haya yatazamwe kwa mujibu wa sheria na sheria zifuatwe lakini pia
kwa kuzingatia haki za binadamu na hususani haki za kiraia na
kiutamaduni ambazo zinatoa uhuru wa ibada na kila mtu asiingiliwe katika
haki hizi.Lakini pia njia za utatuzi wa migogoro ya aina hii isifanywe
kijuujuuu bali pawe na nafasi yamaongezi ya kina ya uchambuzi wa kiini
cha mgogoro.
Tutaweza kutoa taarifa zaidi tutakapopokea taarifa kutoka
kwa waangalizi wetu wa kiini na matokeo ya mgogoro au vurugu hizi
No comments:
Post a Comment