MWANAFUNZI wa Chuo Kikuu cha Bunda kilichopo mijini Lilongwe nchini Malawi,
amejinyongwa kwa kutumia mkanda wa begi lake la kusafiria. Mwanfunzi huyo
aliyetambulika kwa jina la Yobe Magongoninga Mfune (23) alikatisha maisha yake
huku sababu za kifo cha kikiwa siri kati yake na Mungu wake.
Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Malawi Rhoda Manjolo alisema kwamba, Mfune
alikuwa mwanafunzi wa shahada ya kwanza katika fani ya utawala wa mazingira na
maliasiri.
Manjolo alisema, marehemu alikutwa amejinyonga katika chumba chake kwenye
hosteli za chuo hicho. Hata hivyo Polisi walisema kwamba, marehemu alikuwa
na mahusiano na mwanamke mmoja aliyewahi kufanyakazi katika chuo hicho kwa siku
za nyuma.
Msemaji wa Polisi nchini Malawi aliongeza kwamba, marehemiu alikuwa akiishi
na rafiki yake katika chumba hicho ambaye aliondoka tangu may 6 mwaka huu na
aliporudi akakuta mlango umefungwa kwa ndani ndipo alipoamuwa kutoa taarifa kwa
uongozi wa chuo ambao waliamuwa kuvunja mlango huo kuingia ndani.
Alisema kwamba baada ya mlango huo kufunguliwa hawakuona mtu lakini
walipofungua kabati la nguo wakakutana na mwili wa marehemu ukiwa
unaning'ining'ia. "Uchunguzi wa madaktari unasema kwamba kifo cha
mwanafunzi huyo kilitokana na msongo wa mawazo"alisema Manjolo.
Hata hiyo marafiki wa karibu wa mwanafunzi huyo walisema kwamba, siku chache
kabla ya marehemu kufariki dunia aliwahi kuandika katika ukurasa wake wa Face
Book kwamba "nitaweka historia nyingine mpya ambayo sijawai kuiweka tangu
nilipozaliwa, na kumbukukumbu yake haitakaa ikafutika tena,na baada ya hapo sitajali
wala kuwa na mahusiano na mambo yote ya hapa duniani, bali itakuwa juu yangu na
Mungu wangu"ilisema sehemu ya status za marehemu.
No comments:
Post a Comment