Wednesday, January 30, 2013

TAARIFA YA MKUTANO WA M.D.I DAR ES SALAAM ULIOFANYIKA TAREHE 27/01/2013 MARYLAND PUB, MWENGE DSM




AGENDA

1.      UTANGULIZI
2.      KUFUNGUA KIKAO
3.      KUKAMILISHA USAJILI WA UMOJA
4.      MAJUKUMU YA UMOJA KWASASA
5.      KUHAMASISHA MAWASILIANO BAINA YA WAJUMBE
6.      KUHIMIZA UTOAJI WA MICHANGO YA MWISHO WA MWEZI
7.      MENGINEYO
8.      HITIMISHO

1.      UTANGULIZI
Umoja wa Wanamagu ni umoja wa Hiari, usio wa Kiserikali, usio wa Kisiasa wala wa kutengeza faida, wenye malengo ya jumla ya kuwaweka pamoja wananchi wote wa Wilaya ya Magu iliyoko Mkoa wa Mwanza Tanzania kwa dhumuni la Kuelemisha na Kuhamasisha wananchi kuendeleza Utamaduni na Tabia ya kufanya Kazi kwa ushirikikiano unaojenga uwezo wa kujitegemea na kuleta mabadiliko ya maisha bora kwa watu wote katika familia na jamii kwa ujumla ili kujenga Amani,Umoja, Haki, Udugu, Demokrasia, Elimu, Uchumi, Utawala Bora, na Mazingira Nadhifu katika Jamii.

2.      KUFUNGUA KIKAO
Kikao kilifunguliwa na Mwenyekiti wa MDI kuanzia saa Kumi na Nusu jioni, Maryland Pub, Mwenge Dar es salaam.

3.      KUKAMILISHA USAJILI WA UMOJA

Ili M.D.I iweze kujiendesha kikamilifu na kwa ufanisi ilihitajika kusajili umoja haraka iwezekanavyo ili kupata baraka zote kutoka kwenye mamlaka husika ya nchi yetu ya Tanzania. Kwa hivyo kikao kiliwateua wanachama watatu (3) wafuatao kushughulikia na kufuatilia usajili wa MDI.

  1. Juma William Yabeja
  2. Samuel Magoiga
  3. Wilbert Maige

Wanachama hawa walipewa muda wa wiki mbili  (2) kuwasilisha taarifa ya usajili huo.


Kuwa na umoja uliosajiliwa ni vizuri kwa sababu zifuatazo;

KWANZA,umoja utakuwa na nguvu kisheria ya kuweza kushiriki kikamilifu katika shughuli mbalimbali za maendeleo kama tulivyojipangia kama Magu Development Initiative (MDI).

PILI, itatuwezesha kutekeleza majukumu ya umoja ikiwa ni pamoja na kuweza kupata misaada ya wafadhili wa maendeleo ili kusaidia katika kuteleza malengo ya umoja.

TATU, itatuwezesha kutimiza mahitaji ya kikatiba kama yalivyoainishwa kwenye kaatiba ya MDI Ibara ya 9(10.2) inayoelekeza jinsi ya kuwa na vyanzo mbadala vya mapato ya umoja.

NNE, kama jumuiya, tunatarajia kuwa na mipango mikakati ya kukemea kwa nguvu zote dhana ya UCHAWI, Mauaji ya ALBINO, Mauaji ya VIKONGWE, na mengineyo ambayo kwa muda mrefu yamechangia kudumaza maendeleo ya wanaMagu na Magu kwa ujumla.


4.      MAJUKUMU YA UMOJA KWASASA
Kama isemavyo elimu ndio ufunguo wa maisha na wengi wetu ni mashaidi katika hili, kikao kilionelea kuwepo na mkakati maalumu na endelevu kwa ajili ya kusomesha wanaMagu walio na mahitaji (wanaotoka katika familia masikini). Kwa hiyo kutakuwa kunafanyika FUND RAISING kila mwaka kwa ajiri ya kusomesha wanafunzi hao.

Zaidi tulishukuru Mwana Magu mmoja aitwaye WILBERT MAIGE katika kikao hicho kwa kujitolea kusomesha mwanafunzi mmoja mwaka huu (2013) kutoka shule ya sekondari ya kata ya SUKUMA. Kwa hili bado mlango upo wazi kwa ajili ya mdau yeyote atakayeguswa kujitokeza kwa ajili ya kusaidia wadogo zetu wapate elimu dunia.

5.      KUHAMASISHA MAWASILIANO BAINA YA WAJUMBE WA MDI
Pamoja na wajumbe wengi kujuana kupitia facebook tu tulionelea kwamba umefika wakati mwafaka wa wanaM.D.I kuwa tunakutana ktk vikao sehemu mbalimbali tulipo ili tuzidi kufahamiana zaidi kama wanafamilia moja iitwayo (WANAMAGU). Tunaangalia uwezekano wa kupata kiongozi kila Mkoa na Wilaya zetu kwa ajili ya kufanikisha jambo hili.

6.      KUHIMIZA UTOAJI WA MICHANGO YA MWISHO WA MWEZI
Kikao kilionelea kuendelea kuwaomba wajumbe kujitokeza zaidi kwa ajili ya kutoa ada hii ambayo itatumika kujenga M.D.I na sisi pia. Matumizi yake yatolewa kila hela itakapotumika kwa ajili ya shughuri za M.D.I. Kiasi kilichobaki kitawekwa kwenye akaunti yetu No. 01J209830000 CRDB BANK.

7.      MENGINEYO

KWANZA, Kuweka ajira zote zinazotolewa katika vyombo vya habari ndani ya M.D.I ili wadau wapate kuziona na kuomba kazi hizo.
PILI, Kuwa na ofisi kuu Dar Es salaam kama ilivyoainishwa kwenye Katiba.

8.      HITIMISHO
Kama wanamagu na wanachama wa umoja huu wa MDI, tuna jukumu la msingi la kushiriki katika shughuli za kukuza umoja wetu na pia katika shughuli zake kwa kujitoa kwa dhati kimaarifa, muda, kirasilimali na juhudi.

Nawatakia kushiriki kwema kuijenga Magu Mpya.

MAENDELEO YA MAGU…PAMOJA TUNAWEZA

No comments:

Post a Comment